Luke 23:3-8

3 aBasi Pilato akamuuliza Isa, “Wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?”

Isa akajibu, “Wewe wasema.”

4 bPilato akawaambia viongozi wa makuhani na watu wote waliokuwepo, “Sioni sababu ya kutosha kumshtaki mtu huyu!”

5 cLakini wao wakakazana kusema, “Anawachochea watu kwa mafundisho yake katika Uyahudi yote, tangu Galilaya alikoanzia, hadi sehemu hii!”

Isa Apelekwa Kwa Herode

6 dPilato aliposikia hayo akauliza, “Huyu mtu ni Mgalilaya?” 7 eAlipofahamu kwamba Isa alikuwa chini ya mamlaka ya Herode, akampeleka kwa Herode, ambaye wakati huo alikuwa pia Yerusalemu.

8 fHerode alipomwona Isa alifurahi sana, kwa sababu kwa muda mrefu alikuwa amesikia mambo mengi kumhusu yeye. Pia alitarajia kumwona akifanya miujiza kadha wa kadha.
Copyright information for SwhKC