Luke 23:3-8
3 aBasi Pilato akamuuliza Isa, “Wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?” Isa akajibu, “Wewe wasema.” 4 bPilato akawaambia viongozi wa makuhani na watu wote waliokuwepo, “Sioni sababu ya kutosha kumshtaki mtu huyu!” 5 cLakini wao wakakazana kusema, “Anawachochea watu kwa mafundisho yake katika Uyahudi yote, tangu Galilaya alikoanzia, hadi sehemu hii!”Isa Apelekwa Kwa Herode
6 dPilato aliposikia hayo akauliza, “Huyu mtu ni Mgalilaya?” 7 eAlipofahamu kwamba Isa alikuwa chini ya mamlaka ya Herode, akampeleka kwa Herode, ambaye wakati huo alikuwa pia Yerusalemu. 8 fHerode alipomwona Isa alifurahi sana, kwa sababu kwa muda mrefu alikuwa amesikia mambo mengi kumhusu yeye. Pia alitarajia kumwona akifanya miujiza kadha wa kadha.
Copyright information for
SwhKC